• Registered UK Charity 1103895

KISIMA NAMBA 786 CHAKABIDHIWA KATIKA KUENZI SIKU YA KIFO CHA BIBI FATMA ZAHRA (A.S)

KISIMA NAMBA 786 CHAKABIDHIWA KATIKA KUENZI SIKU YA KIFO CHA BIBI FATMA ZAHRA (A.S)

Katika kuadhimisha na kuikumbuka siku ya kifo cha Binti mpendwa wa Mtume Muhammad (S.A.W), Bibi Fatma Zahra (A.S), The Desk and Chair Foundation chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Alhaaj Dokta Sibtain Meghjee, imekabidhi rasmi kisima namba 786 cha maji safi na salama kwa wananchi wa Kijiji cha Katunguru.

Kisima hiki ni sehemu ya juhudi endelevu za taasisi katika kuhakikisha kuwa jamii zilizopo vijijini zinapata huduma ya msingi ya maji safi na salama, ikiwa ni mchango wa moja kwa moja katika kutimiza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), hususan Lengo la 6 – Maji Safi na Usafi wa Mazingira kwa Wote.

Makabidhiano haya yamepokelewa kwa shukrani kubwa na wananchi wa eneo hilo, ambao wameahidi kulitunza kisima hicho kwa matumizi ya vizazi vya sasa na vijavyo. Hili ni tukio muhimu linaloakisi dhamira ya The Desk and Chair Foundation ya kuendeleza matendo ya huruma, ustawi wa jamii, na huduma kwa wote bila ubaguzi.

“Huduma ya maji safi ni sadaka ya kudumu na mojawapo ya njia bora za kumtumikia Mwenyezi Mungu kwa kutumikia binadamu.”

— Alhaaj Dokta Sibtain Meghjee, Mwenyekiti wa The Desk and Chair Foundation
Taasisi itaendelea kujitoa kusaidia jamii kwa njia mbalimbali zinazogusa maisha ya watu moja kwa moja, huku ikidumisha misingi ya utu, mshikamano na maadili ya kijamii.

News & Updates

Join Our Mailing List

Keep up to date with all of our wonderful achievements

Loading